Friday, May 16, 2014


Kabla ya kugombana Nemanja Vidic wakiwa na Evra katika furaha
 
MABEKI wa Manchester United, Nemanja Vidic na Patrice Evra, wameripotiwa kukunjana mashati kabla ya kocha David Moyes kuwagombelezea wakati walipotaka kuzipiga mazoezini kwa hasira zinazotokana na timu kufanya vibaya kwenye Ligi Kuu England msimu uliomalizika hivi karibuni.
Mastaa hao wameripotiwa kutaka kuzipiga baada ya timu yao kuchapwa 3-0 na Liverpool kwenye Ligi Kuu England uwanjani Old Trafford Machi mwaka huu na hivyo kutibua zaidi msimu wao kabla ya kocha Moyes hajatimuliwa na Ryan Giggs kuchukua mikoba.
Kwenye mchezo huo ambao Vidic, alitolewa kwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano na mwamuzi, Mark Clattenburg, alimshutumu Evra kwa kushindwa majukumu yake ya ulinzi kwenye mechi hiyo na kusababisha beki ya Man United kuonekana dhaifu wakati wa mchezo.
Kauli hiyo imeelezwa ilimtibua Evra na kukunjana mashati na beki mwenzake, kabla ya kocha wao kuingilia kati kuwapangua kwenye uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo huko Carrington.
Vidic anaondoka Old Trafford na kwenda kujiunga na Inter Milan baada ya miaka minane aliyodumu Man United.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe