Wednesday, May 7, 2014

Talib amshawishi Malkia wa Nyuki Simba

MWANAMAMA aliyetingisha nchi akiwa na klabu ya Simba, Rahma Al Kharoos ‘Malkia wa Nyuki’ amepigiwa chapuo kuwa anaweza kuiongoza klabu hiyo kwa mafanikio.
Malkia wa Nyuki kiongozi na mjumbe wa Kamati Utendaji ya Simba, ndiyo alikipeleka kikosi hicho nchini Oman kwa ajili ya kambi ya wiki mbili.
Akizungumza na Mwanaspoti, Talib ambaye ni kocha na mchezaji wa zamani wa Simba na mtu wa karibu wa Malkia wa Nyuki kwani wote wanaishi pamoja nchini Oman.
Alisema: “Kwa namna ninavyomjua Rahma (Malkia wa Nyuki) kama ataamua mwenyewe aiongoze Simba, timu itakuwa na mafanikio makubwa kwa sababu ni mpambanaji na anajua kazi. Lakini sijui kama yeye mwenyewe atakuwa tayari kwa namna ninavyojua, huwa ana majukumu mengi kwenye biashara zake na mambo mengine, anaweza asiwe tayari,”alisema Talib.
Hata hivyo, Mwanaspoti ilimtafuta Malkia wa Nyuki ambaye huwa anazunguka nchi mbalimbali kwa sababu ya shughuli zake, haikufanikiwa.
Talib ambaye ni kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Oman ya soka la Ufukweni, alikwenda mbali na kusisitiza, atamshawishi Malkia wa Nyuki ili utakapofika wakati wa uchaguzi, achukue fomu ya uongozi wowote.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe