Wednesday, May 21, 2014

Stori: Adamu Mwanakatwe
KIFO cha nyota wa filamu Bongo, Adam Kuambiana kilitibua  sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya watoto wawili Nicole na Martin iliyoandaliwa na Aunt Ezekiel akiwa na shoga yake Wema Sepetu.
Mastaa hao walikuwa wamekamilisha kila kitu na walishaanza shamrashamra zaa, ghafla wakasikia taarifa za kifo cha Kuambiana.

Nyota wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel
“Mi naumia jamani, unajua filamu yetu ya mwisho tuliyocheza mimi na Wema, yeye alikuwa dairekta. Yaani tulikuwa  tukimchezea kama babu yetu, hebu angalia hii clip,” alisema Aunt huku akimwonyesha mwandishi wetu clip hiyo kwenye simu yake.
Hata hivyo kwa kuwa walikuwa wameshatayarisha kila kitu huku  waalikwa wakiwa eneo la tukio, walimalizia hafla hiyo ingawa  machozi yakitawala badala ya furaha.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe