Thursday, May 8, 2014

Ivo upo? Msikie huyu Mzee Mtemi hapa

MWAMUZI mkongwe nchini Idd Ngongite ‘Mtemi’ ametamka wazi kuwa kama yeye angekuwa anachezesha sasa mechi za Ligi Kuu basi kila mechi angekuwa akimpa kadi za njano kipa wa Simba Ivo Mapunda kutokana na kuingia na taulo lake uwanjani.
Ngongite ambaye alitamba katika miaka ya 70 alisema angeweza kumhukumu kwa sheria namba 4 sheria kati ya zile 17 ambazo zinaonyesha mavazi na vitu ambavyo mchezaji anatakiwa kuingia navyo uwanjani lakini kati ya hivyo taulo halipo.
Akizungumza na Mwanaspoti mjini hapa Ngongite alisema sheria namba 4 ya mavazi kwa mchezaji inajieleza vitu ambavyo anatakiwa kuwa navyo ambavyo ni jezi,glovu na vifaa vingine kama vizuia ugoko lakini, haielezi kuingia na vitu vingine kama taulo.
“Nimeona hata Ulaya waamuzi wanashindwa kuwapa adhabu hawa wachezaji wanaoingia na mataulo uwanjani kwa kuwa kwanza havijakaguliwa na pili sheria namba 4 ya mavazi haijaruhusu. Sasa kama mimi angekuwa anakutana na kadi za njano kila mechi ule ni ubishoo tu taulo anayetakiwa kuna nalo ni daktari wa timu tu,”alisema Ngongite.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe