Tuesday, April 29, 2014

Jaji Samatta, Prof Lumumba kutumika kuwarejesha Ukawa bungeni

 

Huwezi kuwalazimisha watu kuamua jambo ambalo hawalitaki kama ni muundo wa Muungano tunaomba wananchi ndiyo waamue, lakini yote hayo Katiba yetu inatakiwa kubainisha mambo mbalimbali yanayohusu watu wenye ulemavu na haki zao zote,”

Wiki hii Bunge Maalumu la Katiba limeahirishwa, kupisha Bunge la Bajeti kuanza vikao vyake vya bajeti kwa mwaka mpya wa fedha wa 2014/15.
Hata hivyo, Bunge hilo limeahirishwa likiwa limegawanyika vipande, baada ya wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutoka nje ya Bunge hilo Aprili 16, wakipinga kejeli, matusi na mambo mengine ya ukiukwaji wa taratibu yaliyokuwa yakifanywa na baadhi ya mawaziri nje ya Bunge.
Kutoka kwa Ukawa nje unaojumuisha vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, DP na wajumbe 25 kutoka kundi la 201 hakukuzuia Bunge hilo kuendelea na vikao vyake. Bunge hilo limeahirishwa Agosti 5, litakapokutana tena mjini Dodoma kuendelea na majadala wa kuijadili Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba.
Kundi la Tanzania Kwanza linalojumuisha wajumbe wengi wa CCM, wamekuwa wakiwapiga vijembe kuwa warudi bungeni kuendelea na mjadala huo kwani Katiba haitengenezwi nje ya Bunge.
Jukata yasaka suluhu
Kutokana na mgawanyiko huo kuonyesha kuligawa taifa na kuwaacha wananchi wakiwa njiapanda juu ya hatima ya kupata Katiba Mpya, Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) linajipambanua kutaka kusaka suluhu ya mvutano huo.
Mwenyekiti wa Jukata, Deus Kibamba anasema, Jukwaa hilo linajitolea kusaka suluhu kwa kuratibu maridhiano ya makundi yanayovutana ya Ukawa na la Tanzania Kwanza.
Anasema lengo la kusaka maridhiano hayo ni kuhakikisha kabla ya Bunge hilo kuanza Agosti 5, kunakuwapo maridhiano, yatakayowezesha wajumbe wote wanakuwa kitu kimoja katika kujadili maudhui ya rasimu, licha ya tofauti zao za kiitikadi na kimisimamo.
Kibamba anasema wameamua kuwaalika wataalamu ambao wana uzoefu wa siku nyingi katika masuala ya sheria kusimamia maridhiano hayo, yatakayojenga umoja na mshikamano katika taifa.
Wataalamu hao kwa mujibu wa Kibamba ni Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Barnabas Samatta anayekuwa mwenyekiti, Profesa Patrice Lumumba kutoka nchini Kenya ambaye atakuwa msuluhishi mwenza sambamba na uwepo wa makundi ya viongozi kutoka Ukawa, Tanzania Kwanza, vyama vya siasa, asasi za wananchi na taasisi zote muhimu zilizoguswa na mchakato huu.
“Katika kujenga Katiba yenye kuwajali wananchi, tunaomba kila upande kuridhia kukutana na kutokuwa na misimamo mikali ili kuhakikisha tunawaunganisha na kuendelea na mchakato huo kama kawaida,” anasema Kimbamba.
Kuhusu uhalali wa Bunge hilo kuendelea na mijadala licha ya Ukawa kutoka nje, anasema sheria za Jumuiya ya Madola kwa mabunge ya Katiba kundi moja linapotoka nje kwa tamko, Bunge hilo hutakiwa kusitishwa

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe