Saturday, February 1, 2014

Ronaldo ashitua kumwita Irina mkewe

Ronaldo akiwa na mpenzi wake, kwenye tuzo za mwanasoka bora wa dunia  

SUPASTAA, Cristiano Ronaldo ameibua mapya kwenye sherehe za utoaji wa Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa Mwaka zilizofanyika Uswisi Jumatatu iliyopita baada ya kumtambulisha mpenzi wake, mrembo Irina Shayk kuwa ni mkewe.
Utata ulioibuka kama staa huyo wa Real Madrid kama atakuwa amemuoa kwa siri mrembo huyo wa Kirusi anayejihusisha na masuala ya mitindo.
Ronaldo baada ya kutajwa mshindi na kuwabwaga wapinzani wake, Lionel Messi na Franck Ribery kwenye hotuba yake ya kushukuru, alimtaja Irina kuwa mkewe jambo lililowashitusha wengi ukumbini hapo.
Mreno huyo aliaambatana na Irina kwenye tuzo hizo pamoja na mtoto wake na alipotajwa tu kuwa ameshinda, alimbusu mpenzi wake kwanza kabla ya kwenda jukwaani na mwanaye, Cristiano Jr kuwashukuru wachezaji wenzake, familia na “mkewe”.
Ronaldo alisema: “Namshukuru kila mtu aliyehusika na mimi kwenye viwango tofauti. Mke wangu, marafiki zangu na mwanangu. Hili ni tukio lenye hisia kubwa.”
Ronaldo amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mrembo huyo wa Urusi tangu 2010.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe