JE,MWAMUZI ALIKUWA SAHIHI KUIPA PENATI MAN CITY PAMOJA NA KUMPA KADI NYEKUNDU BEKI DANNY ROSE?
Mwamuzi msaidizi Scott Ledger jana usiku alikuwa na mchango mkubwa kwenye mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu nchini England baada ya kutoa maamuzi tata yaliyoisaidia Manchester City kuifunga Totenham mabao 5-1
Kwenye mchezo huo mwamuzi huyo
aliipa Man City penati ambayo haikustahili kutokana na beki wa Spurs Danny Rose
kuucheza mpira kwanza kabla ya mshambuliaji Edin Dzeko hajaanguka chini.
Maamuzi hayo yalipelekea beki huyo
kupewa kadi nyekundu ikiwa ni pamoja na adhabu ya penati ilikwamishwa wavuni na
Yaya Toure.
0 comments:
Post a Comment